Saturday, 14 January 2012
Friday, 13 January 2012
Thursday, 12 January 2012
KONA YA MAPISHI
CHAPATI ZA KUKU
VIPIMO
Kuku wa kusaga 1lb
Nyanya 1 ndogo
Thomu 1½ kijiko cha chai
Tangawizi 1 kijiko cha chai
Pilipili manga 1 kijiko cha chai
Bizari unataka ½ kijiko cha chai
Kidonge cha supu 1
Pilipili mbichi 1 au 2
Chumvi kiasi
Vitunguu vya majani kiasi
Vitunguu 2
Mayai 6
Manda za tayari (spring rolls) 12
Nyanya 1 ndogo
Thomu 1½ kijiko cha chai
Tangawizi 1 kijiko cha chai
Pilipili manga 1 kijiko cha chai
Bizari unataka ½ kijiko cha chai
Kidonge cha supu 1
Pilipili mbichi 1 au 2
Chumvi kiasi
Vitunguu vya majani kiasi
Vitunguu 2
Mayai 6
Manda za tayari (spring rolls) 12
NAMNA YA KUTAYARISHA
1. Saga nyanya, thomu, tangawizi na pilipili kwenye blender
2. Tia kima, vitu ulivyosaga, pilipili manga,kidonge cha supu, chumvi na bizari.
3. Weka motoni huku ukichanganya mpaka ikauke.
4. Kisha iache pembeni ipoe.
5. Kisha kata kata vitungu Kama vya sambusa na vitungu vya majani.
6. Chukuwa bakuli tia kima kama vijiko 4 au zaidi vya supu
7. Tia vitunguu vyote aina mbili kiasi na mayai mawili.
8. Chukuwa sinia ya oveni tia mafuta kama vijiko 2 au zaidi kidogo
9. Kisha panga manda 2 kwenye sinia.
10. Changanya mchanganyiko kwenye bakuli mimina juu ya manda utandaze.
11. Kisha funika manda 2 nyingine kwa juu na waweza kufanya 3 kwa pamoja.
12. Choma kwenye oveni moto wa chini ikishaiva tia mafuta geuza upande wa pili epua na itakuwa tayari kuliwa.
2. Tia kima, vitu ulivyosaga, pilipili manga,kidonge cha supu, chumvi na bizari.
3. Weka motoni huku ukichanganya mpaka ikauke.
4. Kisha iache pembeni ipoe.
5. Kisha kata kata vitungu Kama vya sambusa na vitungu vya majani.
6. Chukuwa bakuli tia kima kama vijiko 4 au zaidi vya supu
7. Tia vitunguu vyote aina mbili kiasi na mayai mawili.
8. Chukuwa sinia ya oveni tia mafuta kama vijiko 2 au zaidi kidogo
9. Kisha panga manda 2 kwenye sinia.
10. Changanya mchanganyiko kwenye bakuli mimina juu ya manda utandaze.
11. Kisha funika manda 2 nyingine kwa juu na waweza kufanya 3 kwa pamoja.
12. Choma kwenye oveni moto wa chini ikishaiva tia mafuta geuza upande wa pili epua na itakuwa tayari kuliwa.
Tuesday, 10 January 2012
WASAIDIE WATOTO HAWA
KATIKA gazeti la Uwazi, toleo la wiki iliyopita walitoa habari za mtoto Mustafa Ally, 12, (pichani), mkazi wa Mtoni Mtongani, Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam anayewauguza wadogo zake mapacha wenye umri wa miezi nane.
Mtoto Mustafa ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Twiga, Temeke amelazimika kuwauguza wadogo zake hao, Swaumu na Ramadhani kwa kuwa baba yao alishafariki na mama yao yupo mahututi.
Watoto hao mapacha wanaumwa na wamelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu. Mama yao aliyekuwa akiwauguza aliugua ghafla na kupewa matibabu na kwa sasa yupo hoi nyumbani kwake, hivyo Mustafa kuchukua mzigo huo wa kuwauguza.
Matatizo yanayoikabili familia hiyo ni pamoja na ukosefu wa chakula, nguo za kawaida na za shule, fedha za matumizi, maziwa ya unga ya watoto na kodi ya nyumba.
Gazeti hilo kwa niaba ya familia hiyo linatoa shukrani kwa watu mbalimbali waliompatia msaada wa maziwa, sabuni, sukari, nguo na fedha, vyote vikiwa na thamani ya shilingi 300,000.
Bado msaada unakaribishwa kwa watoto hawa. Aliyeguswa na kilio cha mtoto Mustafa afanye mawasiliano na Afisa Ustawi wa Jamii Muhimbili, Erika Ishengoma kwa simu 0714 220 038 au mwandishi wetu kwa namba 0713 454 656 au afike Muhimbili wodi ya watoto, Makuti B atakutana nao ana kwa ana.
E'M E'M GET 2GETHER'Z PARTY .............@CINE CLUB
Karen & Kulwa (wakurugenzi)
Zuhura
Rehema....mamaa wa NOVA'S CHOICE
Tamali
Miriam
Karen, Kulwa & Benedicta
makulaajii
na hili ndilo kundi la E'M E'M Dar es salaam branch
WAKAZI WA UINGEREZA WACHANGIA WALIOATHIRIKA NA MAFURIKO TANZANIA
Louisa
Frisch (Bright Future TZ), Jestina George, Haruna Mbeyu (TA London)
& Chris Lukosi 'Mzee wa Kazi (Serengeti Freight)
Umi Macho, Jestina George & Louisa
Jestina akimshukuru Pr. Mattheww kwa mchango wake
Mzee wa Kazi Chris Lukosi, Louisa (Bright Future TZ), Jestina George & Pastor Matthew
Haruna Mbeyu, Mzee wa Kazi (Serengeti Freight) Mohsin akimpa mkono wa shukran Naibu Balozi
Mzee wa kazi (serengeti Freight) Chris Lukosi na Naibu Balozi
Katibu wa CCM East London & Katibu wa TAWA UK Mariam Mungula akiwa na
Baadhi
ya viongozi wa TA London Haruna Mbeyu, Said Surur wakiwa katika picha
ya pamoja na Naibu Balozi na dada Louisa wa Bright Future TZ
Wazee wa kazi 'Kikazi Zaidi'
Chris akimshukuru Iscandar kwa support yake
Viongozi wa TA London wakiwa katika picha ya pamoja na waandaji wa hrambee
Hivi ni baadhi ya vitu vilivyo patikana katika Harambee
Said Suru, Dullah Meru, Iscandar, Chris Lukosi & Jestina katika picha ya pamoja
Picha ya pamoja baada ya shughuli kuisha na baadhai ya wadau waliojitokeza kuchangia
---
Siku
ya Jumamosi tarehe 7 January 2011 Serengeti freight wakishirikiana na
Miss Jestina Blog, Bright Future TZ pamoja na Urban Pulse walifanya
harambee maalum ya kuchangia watanzania walioathirika na mafuriko
yaliotokea hivi karibuni mwishoni mwa mwaka jana nyumbani Tanzania.
Mgeni
rasmi alikuwa Naibu balozi Mh Chabaka Kilumanga. Aidha Mh Balozi
aliongea na kushukuru watanzania wote walioguswa na kujitolea kwa hali
na mali ili kuweza kusaidia watanzania wenzao waliokumbwa na janga hili.
Misaada bado inaendelea kupokelewa na kukusanywa mpaka mwisho wa mwezi
huu wa january. Hivyo basi kwa wale wote walioshindwa kuweza kufika siku
ya jumamosi kutoa michango bado nafasi ipo. Kumbuka hili ni janga letu
wote tafadhali fanya sehemu yako kwa jinsi Mungu anavyokubariki.
KWA MAWASILIANO ZAIDI KUHUSU MISAADA WASILIANA NAJESTINA GEORGE 07404332910FRANK EYEMBE 07865594576BARAKA NYAMA 07816981577
KAMA UNA MCHANGO UNAWEZA KUDEPOSIT KATIKA ACCOUNT IFUATAYO:
BARCLAYS BANK
JINA: TANZANIA ASSOCIATION LONDON Account Number: 23374815
Sort Code: 20-72-89
ANDIKA JINA LAKO NA MAFURIKO AS REFERENCE
TUNAWASHUKURU NYOTE KWA KUJALI NDUGU ZETUContact us for more info;CHRIS LUKOSI 07903828119SIMON LOUIS (MOHSIN) 07950689243BRIAN (BABA NJOROGE) 07795160757HASSAN (RICHARD) 07405159255HQ - UNIT 92 THAMES INDUSTRIAL PARK, PRINCESS MARGARET ROAD, EAST TILBURY, RM18 8RHRHTell (+44) 01375 855917 Fax (+44) 01708202477
Subscribe to:
Posts (Atom)