Pages

Ads 468x60px

Tuesday 1 November 2011

kona ya mapishi

Saladi Ya Bilingani Na Parsley

Vipimo

 Bilingani                                                        3  

Matango                                                       3

Nyanya/tungule                                            3

Kitunguu                                                       2

Parsley (aina ya kotmiri)                               5 misongo (bunches)

 Mafuta ya kukaangia
  

Namna Ya Kutayarisha
 
  1. Katakata bilingani vipande vya  mraba (cubes) kisha kaanga katika mafuta.

  1.  Epua na chuja mafuta kisha weka katika bakuli la saladi.

  1. Katakata matango, nyanya/tungule, kitunguu.

  1. Katakata parsely kisha changanya vizuri.

  1. Wakati wa tayari kula tia dressing (sosi ya saladi)  

Vipimo Vya  Sosi Ya Saladi (Salad Dressing)


Kitunguu thomu                                  3 chembe

Pilipili mbichi                                        1

Siki au and ndimu                                3 vijiko vya supu

Chumvi                                              kiasi

           
Namna Ya Kutayarisha


  1. Chuna (grate) au saga kitunguu thomu, kisha weka katika kibakuli.

  1. Katakata pilipili mbichi (chopp) tia kwenye bakuli

  1. Changanya na viungo vilobakia.

Wakati wa kula, mwagia juu ya saladi uchanganye vizuri ikiwa tayari.

No comments: