Pages

Ads 468x60px

Tuesday 12 June 2012

KONA YA MAPISHI

Nyanya Za Mshumuaa/Chungu/Ngogwe Za Nazi 

  


Vipimo
Nyanya chungu                                   20-25
Tui la nazi                                         1 ½  kikombe
Kitunguu maji                                    ½
Tungule (Nyanya)                               2
Kitunguu Thomu                                 1 kijiko cha sukari
Bizari                                                ¼ kijiko
Chumvi                                              kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
1.     Kosha nyanya chungu kisha zimenye uzipasue kati kati kwa urefu, itasaidia kuona kama hakuna wadudu ndani.

2.     Kata kitunguu maji vipande vidogo vidogo, menya tungule maganda ukate pia.

3.     Kwenye sufuria changanya vitu vyote , weka jikoni upike.

4.     Ikikaribia tui kukauka epua.

5.     Pakua kwa kijiko moja moja ili zisivurugike weka kwenye sahani tayari kuliwa

No comments: