Pages

Ads 468x60px

Thursday, 22 December 2011

MAFURIKO MAFURIKO .............. DAR ES SALAAM

Diys Blog inatoa pole kwa familia za watanzania 13 waliopeteza maisha yao katika mafuriko makubwa yaliotokana na mvua ambazo zimekuwa zikinyesha tokea juzi Jumanne Desemba 20, 2011, Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema peponi Amina. Pia tunatoa pole kwa walioumia na kupoteza mali zao katika mafuriko haya. 

Watanzania, waathirika wa mafuriko wanahitaji michango yetu kwa hali na mali kwa chochote kile ulichojaaliwa, kwa sasa waathirika hao wamejikusanyika shule mbalimbali za msingi na sekondari, vituo vya kupeleka misaada hiyo kwa sasa ambavyo vinajulika ni :-
- Azania Sekondari
- Magomeni
- Msimbazi
- Mchikichini
- Kibasila
- Magomeni
- Uhuru mchanganyiko
- Hananasifu
- Rutihinda
 inahuzunishaje!

                                         siyo jangwani peke yake hapa ni kitunda

                                    barabara nyingi zilikuwa zimefungwa

Wednesday, 21 December 2011


DRESSED BY UNIQUE PEARL COLLECTION.......@IBM PARTY

                                    Myler ndani ya kivazi kutoka Unique Pearl Collection
                                                      Samia Gonga....kivazi UPC
                                                         Devota kivazi ...UPC

 


KONA YA MAPISHI

Kuku Wa Tanduuri

 VIPIMO

 Kuku                                                      5 pounds  (vipande 20 – 25)
Ukwaju                                        ½  pakti ( kwa kikombe kimoja cha maji)
Vitungu thaumu                                              1 kijiko kikubwa cha kulia
Tangawizi                                                        1 kijiko kikubwa cha kulia
Uzile (binzari nyembamba ya unga)              1 kijiko cha chai
Pilipili manga                                                   1 kijiko cha chai
                                                                        (unaweza   kuongeza ukipenda) 
Chumvi                                                            kiasi 
Tandoori masala                                           1 kikubwa cha chai

NAMNA YA KUTAYARISHA .

1.   Watoe ngozi  na wasafishe vizuri halafu wachuje.
2.   Loweka ukwaju na maji kiasi cha kikombe kimoja  uvuruge mpake upate urojo mzito, uchuje kama tui la nazi kutoa kokwa kisha umimine urojo kwenye kuku.  
3.  Tia vitungu saumu na tangawizi vilivyosagwa changanya vizuri na kuku na urojo wa ukwaju.
4.  Kisha tia pilipili manga na uzile na chumvi.(chumvi unaweza kuongeza kidogo kwani wakati wa kuchoma kuku watachuja maji hivyo weka ya kutosha).
5. Tia tandoori masala  changanya
6. Changanya vizuri na waache wakolee kama nusu saa(dakika 30 hivi)

NAMNA YA KUWACHOMA.
  
1.       Kama una oven ya kawadia basi wapange kuku kwenye nyavu ya juu ya oven na weka treya tupu kwenye nyavu ya pili.
2.      Kwenye kifungo cha selector, weka grill na kwenye kifungo cha temperature weka grill vile vile na watachomeka kwa moto wa juu.
3.      Waache wachomeke kama dakika 25 hadi 30 hivi, huku watakuwa wanachuja maji na yatakuwa yanadongoka kwenye treya tupu.
4.      Wakishakauka na kubadilika rangi vizuri, ondoa treya ya maji yaliyotoka kwenye kuku.
5.       Kisha badilisha kifungo cha selector weka bake na kwenye kifungo cha temperature weka 350º weka kama dakika 10 hadi 15 watachomeka kwa moto wa chini.
6.      Kubadilisha vifungo na moto wa kuchomea kunasaidia kuku kuchomeka pande zote mbili bila ya kugeuza geuza.
7.       Wakishakauka vizuri watoe, panga kwenye sahani na saladi au pilipili ya kusaga, au chatine. Tayari kwa kuliwa.

Monday, 19 December 2011

DIAMOND'Z NIGHT @UWANJA WA NYUMBANI........THE PIT STOP

                                                                 Ahmed and Salama
                                                                      Lulu and friend
                                                                 Jestina and mii
                                                                      Salama and I
                                                            Lilly, Rama and Salama
                                                       Lulu unique pearl collection
                                                          Johari, Abdulrahman and I
                                                                  mii and my braza
                                                             Sare sare mauwaaa


MAKAMUZI TIME




ZE LEGZ



 

Friday, 16 December 2011

HONGERA SAANA.....BAHIYYA ABBAS JAYLAN

                                 kwa kula nondo ya uhasibu @Mzumbe University

Thursday, 15 December 2011

VODACOM MISS TANZANIA 2011 AKABIDHIWA GARI LAKE LEO

 Vodacom miss Tanzania Salha Israel akipokea funguo ya gari aina ya jeep patriot lenye thamani ya shilingi milioni 72 ,kutoka kwa meneja matukio na udhamini wa kampuni ya vodacom Tanzania Rukia Mtingwa
                                         Salha akionyesha ufunguo wa gari
    Salha (my binti) akiondoka na gari lake mara baada ya kukabidhiwa (kwenye kona nshaaaaa)

PICHA AKHSANTE  MICHUZI

Tuesday, 13 December 2011

ilivyokuwa j.mos miaka 50 ya uhuru......... London

Diamond
                                                                       Professor J

                                                                     Ali Kiba



                                                                  mh. Balozi
maam Kayla na Julieth
                                                              Lilly na Racheal

                                                                  Johari na Lilly
Salama,Jessica,Julieth na Swaumu
                                                                   Munna na rafikize

 
                                                          Nyusoz'..... Racheal na Johari
Na akiripoti kutoka greenwhich ni ...maaam Kayla!